Makabidhiano
Wananchi na watendaji mbalimbali wilayani Makete Mkoani Njombe wameombwa kutoa ushirikiano kwa serikali iliyopo madarakani ili ilete maendeleo yaliyokusudiwa kwa taifa kama ilivyoahidiwa wakati wa kampeni
Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Veronica Kessi wakati wa makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo aliyemaliza muda wake Mh Daudi Yassin hapo jana
Mh Kessi amesema kwa sasa ni muda wa kufanya kazi na si wakati wa siasa hivyo kwa ushirikiano wa pamoja kutawezesha wilaya ya Makete kusonga mbele kimaendeleo suala ambalo linahitajika katika serikali ya awamu ya 5
Mkuu wa wilaya aliyemaliza muda wake Mh Daudi Yassin amemueleza mkuu mpya wa wilaya kuwa wakati wa uongozi wake yapo baadhi ya mambo ambayo hakuweza kuyamaliza ingawa bado yanaendelea na utekelezaji ikiwemo maboresho ya shamba la mifugo la Kitulo, Mgogoro wa ardhi katika baadhi ya vijiji pamoja na matumizi ya soko lililopo Ngiu Makete mjini
Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Veronica Kessi wakati wa makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo aliyemaliza muda wake Mh Daudi Yassin hapo jana
Mh Kessi amesema kwa sasa ni muda wa kufanya kazi na si wakati wa siasa hivyo kwa ushirikiano wa pamoja kutawezesha wilaya ya Makete kusonga mbele kimaendeleo suala ambalo linahitajika katika serikali ya awamu ya 5
Mkuu wa wilaya aliyemaliza muda wake Mh Daudi Yassin amemueleza mkuu mpya wa wilaya kuwa wakati wa uongozi wake yapo baadhi ya mambo ambayo hakuweza kuyamaliza ingawa bado yanaendelea na utekelezaji ikiwemo maboresho ya shamba la mifugo la Kitulo, Mgogoro wa ardhi katika baadhi ya vijiji pamoja na matumizi ya soko lililopo Ngiu Makete mjini