Mganga matatani kwa kuuza dawa za Serikali kwenye duka lake binafsi.

MKUU wa wilaya Geita Hermani Kapufi , amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Geita Alli Kidwaka kumuondoa mara moja mganga wa Zahanati ya Karoro wilaya na mkoa wa Geita Daniel Zengo , kwa madai ya kuuza dawa za Serikali kwenye duka lake binafsi.

Amesema hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika kwenye Stand mjini Katoro lengo likiwa ni kujadili shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi.

Kapufi amesema kuwa mganga huyo anatakiwa kuondoka kwenye kituo hicho na kufunga duka lake mara moja huku akiagiza kamati ya ulinzi na usalama kufuatilia.

Naye mganga mkuu wa Hospitali ya wilaya ya Geita amekili kuwepo kwa changamoto hizo na kuahidi kunza kuzitatua


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo