Wananchi Wajitolea kutengeneza barabara kwa majembe ya mikono

Wananchi wa mtaaa wa Ruhuwoiko kisiwani manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wameamua kutengeneza barabara kwa majembe ya mikono kwa kung’oa miti baada ya manispaa kuzitelekeza barabara za mitaa kwa miaka mingi bila kuzitengeneza.kutoka Songea tupate taarifa Zaidi.

  blog hii imeshuhudia wananchi hao wake kwa waume wakikata miti na kuiondoa wamesema wamejitolea kutengeneza barabara kwa nguvu zao kutokana na mtaa huo kukosa barabara za kupita gari na kwamba wamechoka kuitwa mtaa wa mazagazaga usio na miundombinu maji na barabara.

Kutokana jitihada na majitoleo ya wananchi diwani wa kata ya Ruhuwiko Wilbert Mahundi amesema baada ya wananchi kujitolea nguvu zao atahakikisha kupitia kiasi kidogo cha fedha zlizootolewa na manispaa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya kata ya Ruhuwiko anapeleka katapila la kukwangua barabara mapema iwezekanavyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo