Unyama unyama: Wananchi wamchoma moto Mtuhumiwa wa Wizi Makete (Audio)

Kufuatia Mauaji ya kutisha na ya kinyama yaliyokithiri wilayani Makete mkoani Njombe wananchi wametakiwa kutojichukulia sheria mkononi na badala yake wawe na hofu ya Mungu

Hiyo inafuatia Tukio la kikatili lililotokea usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Usungilo kata ya Mang’oto wilayani Hapa ambapo wananchi wenye hasira kali  wamemuua kwa kumchoma moto Bw. Silvester Mbilinyi anayekadiriwa kuwa na miaka 25 kwa tuhuma za wizi

Tukio hilo la kusikitisha limekuwa ni mfululizo wa Matukio mabaya zaidi kutokea wilayani Makete kwa kipindi cha Mwezi huu

Hamfrey Msigwa mtendaji wa kijiji cha Usungilo amesema mtuhumiwa huyo alibomoa vibanda vya biashara vya watu watatu mnamo tarehe 21 June 2016 na anaelezea tokea kuanza kwa tukio mpaka mwishowe umauti unamkuta mtuhumiwa

Daktari kutoka Hospitali ya wilaya ya Makete Idrisa Kilanga amethibitisha mauaji hayo na kusema kwamba aliyekufa ni wa Jinsi ya Kiume na amechomwa moto huku sura yake haijulikani vizuri kutokana na kuungua vibaya

Jeshi la polisi limefika eneo la tukio mnamo saa 12:00 jioni ya jana na kushuhudia majivu mahali mauaji yalipotokea jirani na ofisi ya Afisa Mtendaji wa kijiji cha Usungilo na kwenda Makaburini kuona mwili wa Marehemu aliyeunguzwa vibaya na kutoa wito kwa Raia kutojichukulia sheria Mkononi kwani hali hiyo inasababisha kuvurugika kwa Amani Wilayani Makete

Sikiliza sauti hapa chini


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo