Wananchi wa kijiji cha Masisiwe kata ya Ukwama Wilayani Makete mkoani Njombe wamefanikiwa kujenga vyoo bora kwenye nyumba za walimu kwa kushirikiana na serikali ya kijiji hicho.
Hayo yamebainishwa na Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw.Danford Sanga wakati akizungumza na mwandishi wetu.
Amesema kuwa ujenzi huo ulianza mapema mwaka huu na kila mwananchi alichangia kiasi cha shilingi elfu tano na kila choo kiligharimu kiasi cha shilingi milioni moja na laki tano.
Bw. Sanga amaeiomba serikali iwasaidie ili waweze kukamilisha ujenzi huo.
Pia amewapongeza wananchi wa kijiji cha Masisiwe kwa kujitoa kujenga vyoo hivyo bora vya walimu na kuwaomba wale ambao bado hawajajenga vyoo bora nao wajenge katika nyumba zao.
Hayo yamebainishwa na Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw.Danford Sanga wakati akizungumza na mwandishi wetu.
Amesema kuwa ujenzi huo ulianza mapema mwaka huu na kila mwananchi alichangia kiasi cha shilingi elfu tano na kila choo kiligharimu kiasi cha shilingi milioni moja na laki tano.
Pia amewapongeza wananchi wa kijiji cha Masisiwe kwa kujitoa kujenga vyoo hivyo bora vya walimu na kuwaomba wale ambao bado hawajajenga vyoo bora nao wajenge katika nyumba zao.