Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rajab Rutengwe (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Steven Kebwe (kushoto) wakiwa katika tukio rasmi la makabidhiano ya ofisi lililofanyika Machi 24, 2016.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyemaliza muda wake, Dk. Rajab Rutengwe amemuomba msamaha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. John Pombe Magufuli kwa kushindwa kuendana na kasi ya "HAPA KAZI TU" hali iliyopelekea kuwekwa pembeni na nafasi yake kuchukuliwa na Dk. Kebwe Kebwe, ambapo amemuomba amfikirie upya kutokana na kutokujua pa kushika baada ya kuwekwa kando.
Dk. Rutengwe Aliyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi ofisi kwa Mkuu mpya wa mkoa huo, Dk Kebwe S. Kebwe
angalia video hii hapa chini