Ishu ya mjamzito kujifungua chooni yafika "pabaya"

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk. Grace Maghembe ameunda kamati kuchunguza tukio la mjamzito mkazi wa Tabata Kisiwani, Asha Sudi (17) kudaiwa kujifungulia mtoto chooni katika Hospitali ya Amana. 

“Tumepata taarifa hizo na tayari tumeanza uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo, tukishakamilisha tutatoa tamko,” alisema. 

Juzi, Mganga Mkuu wa Amana, Dk Meshack Shimwela alikaririwa akisema hakuona kosa kwa muuguzi kumuambia mjamzito huyo kwenda kuoga wakati akiwa na uchungu wa kujifungua. 

Mzazi huyo alisema alipofika mapokezi katika hospitali hiyo hakupimwa chochote, badala yake aliambiwa na muuguzi aende bafuni kuoga na kubadilisha nguo. 

Baadhi ya madaktari waliobobea katika uzalishaji wajawazito walisema kitendo hicho hakikuwa sahihi kwa kuwa mjamzito anapokuwa kwenye hali ya kuumwa uchungu hapaswi kwenda kuoga bila uangalizi wa mtalaamu wala kufanyiwa vipimo. 

“Kuoga ni jambo la kawaida kwa mjamzito, lakini anapokuwa kwenye uchungu wa kujifungua huwa hajitambui na anaweza kufanya vitu ambavyo vitahatarisha uhai wa mtoto au yeye mwenyewe,” alisema daktari ya wodi ya wazazi wa Hospitali ya Mkoa wa Geita, Makoye Mayenga. 

Mtaalamu wa magonjwa ya wanawake na uzazi wa Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi Muhimbili, Dk Sariel Massawe alisema mjamzito anapokuwa katika hali hiyo anatakiwa kufanyiwa vipimo ili kujua uchungu wake uko katika hatua gani. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo