Tukio hilo la kusikitisha la mauwaji ya mtoto huyo lilitokea hapo jana majira ya saa moja na nusu usiku katika mtaa huo wa mji wa zamani mjini hapa na lilisikitisha watu wengi wa Manspaa ya mji wa Mpanda.
Mwenyekiti wa Mtaa huo Magreti John alimweleza mwandishi wa gazeti hili aliyekuwepo kwenye eneo hilo la tukio kuwa alipata taarifa za kuuawa kwa mtoto huyo ambae alikuwa akiishi na baba wake wa kambo aliyekuwa amemuowa mama yake Suzana Elias.
Alisema baada ya kupata taarifa hizo kutoka kwa wangaji wa nyumba hiyo alifika kwenye nyumba hiyo na ndipo walipomweleza kuwa kuna mtoto ameuawa na wazazi wake na wamemfungia ndani wakiwa wameuficha mwili huo wa marehemu kwa muda wa siku tatu.
Mwenyekiti huyo wa mtaa alieleza wapangaji hao walishitushwa baada ya kuona mtoto huyo kutoonekana kwake kwa muda wa siku tatu na chumba walichokuwa wakiishi wanandoa hao kuanza kutowa harufu ya kitu kilicho oza na kila walipoulizwa mtoto wao yuko wapi walionekana wanandoa hao kuwa na mashaka na walijibu kuwa mtoto wao anaumwa.
Ndipo walipoamua kutowa taarifa kwa mjumbe wa serikali ya mtaa anaeitwa Matha Idd ambaye naye alitowa taarifa kwa kwake yeye Mwenyekiti wa mtaa ambae aliwapatia tarifa jeshi la Polisi na waandishi wa Habari .
Polisi walifika kwenye eneo hilo na kukuta kundi la watu huku wakiwa na silaha za jadi mawe na fimbo wakiwa wameizingira nyumba hiyo kwa lengo la kutaka kuwashambulia wanandoa wengine huku wengine wakiwa wamshika mafuta ya taa kwa lengo la kutaka kuchoma nyumba hiyo .
Askari polisi ambao walikuwa na silaha za moto walifanikiwa kuwatawanya wananchi hao na kasha waliingia ndani ya chumba na kuwachukua wanandoa hao wawili na kuwapeleka kituo cha polisi cha Mpanda mjini huku wananchi hao wakiwasindikiza kwa kuwarushia mawe.
Kisha polisi waliokuwa wamebaki hapo pamoja na mwenyekiti wa mtaa walifnya uchunguzi wa awali wa kuukagua mwili wa marehemu mtoto huyo na waliweza kuukuta ukiwa umechomwa na moto kichwani na mikononi huku ukiwa umeanza kuharibika na ukiwa unatowa maji mwilini.
Mmoja wa wanandoa hao aliyejitambulisha kwa jina la Maria Komba alieleza kuwa kabla ya tukio hilo amekuwa akisulisha ugomvi wa mara kwa mara ambapo Juma Selemani alikuwa akipinga kitendo cha mke wake kuishi nyumbani kwake marehemu na alikuwa akimtaka mkewe ampeleke kwa baba yake mzazi kwani yeye alikuwa akidai hawezi kukaa na kumtunza mtoto ambae sio wake .
Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi wa Mkoa wa Katavi Mohamed Rashid I amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la kusikisha .
Alisema wanandoa hao wote wawili wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi na watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika.
- Taarifa ya Walter Mguluchuma - Katavi Yetu blog