Lori lafunga barabara Ikonda Makete....watumiaji wakiona cha Mtemakuni

Abiria waliokuwa wakisafiri kutoka na kwenda Njombe na mkoa jirani wa Mbeya pamoja na watumiaji wengine wa barabara, jana wamekiona cha moto baada ya kusota eneo la Luchala kijiji cha Ikonda kata ya Tandala kwa zaidi ya saa 8 kutokana na lori lililokuwa limebeba mali za serikali kukwama na kuziba barabara

Tukio hilo la aina yake limesababishwa na ukubwa wa lori hilo hasa ukizingatia kwamba udogo wa Makete ni wa mfinyanzi na hivyo kuwa na utelezi hasa ukinyeshewa na mvua kama ilivyotokea jana

hata hivyo lori hilo lilivutwa eneo hilo majira ya saa nne usiku na kusababisha mawasiliano ya barabara hiyo kurejea kama kawaida, huku abiria wakitumia bodaboda kwenda kwenye maeneo wanayotaka kufika pamoja na mabasi yaliyokuwa ng'ambo ya pili kulazimika kurudi na abiria yalikotoka, hasa yaliyokuwa yakienda Makete mjini

Hizi hapa chini ni picha za tukio hilo
 abiria wakitembea kwa miguu kutafuta usafiri wa kuwafikisha Makete mjini na Bulongwa
Basi la Mwafrika likiwa limesimama baada ya kushindwa kupita eneo hilo
 Lori lililofunga barabara baada ya kukwama
 kazi kweli kweli
 Abiria wakiangalia nafasi kwenye basi hili



 Wazee wangu hawa daaah hadi huruma, ni mwendo wa kutembea kwa miguu
 Barabara ndio imefungwa kwa namna hii
 Bodaboda nayo ikiteleza kwenye eneo hilo
 Wanafunzi wakitembea kwa miguu angalau wawahi wakaripoti shuleni



 Gari dogo likijitahidi kupenya pembeni mwa lori lililofunga barabara


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo