Taarifa mpya kuhusu afya ya Spika Job Ndugai kutoka India

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai ameeleza kusikitishwa na taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na katika baadhi ya vyombo vya habari zikieleza kuwa ni mgonjwa mahututi.

Akizungumza juzi kwa simu kutokea India, mmoja wa wasaidizi wa Ndugai, Lukindo Choholo, alisema taarifa hizo zimemsikitisha kwa sababu anaamini wanaozisambaza wana lengo la kupotosha jamii.

Choholo alisema Ndugai ambaye yuko nchini India kwa uchunguzi wa macho, amekuwa akifuatilia taarifa zinazomhusisha na kuugua maradhi ya figo na ini, huku wanaozisambaza wakiwa hawana taarifa za uhakika kuhusu mwenendo wa afya yake.

“Habari zinazosambazwa huko nyumbani kwenye mitandao ya kijamii na kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuwa Spika Ndugai ni mgonjwa sana zinamsikitisha sana, anafuatilia kwenye mitandao na magazeti pia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo