Rais Magufuli awasimamisha kazi maafisa wa TAKUKURU Waliosafiri nje ya nchi bila kibali

Katika hatua nyingine katibu mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema, Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi waandamizi wanne wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU ambao walisafiri nje ya nchi licha ya Rais Magufuli kupiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari kutoka kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Balozi Sefue amewataka watumishi wengine wa umma kutii agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kuonya kuwa atakayekiuka atachukuliwa hatua kali.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
16 Desemba, 2015

BONYEZA PICHA HAPO CHINI KUSIKILIZA SAUTI YA IKULU KUHUSU UAMUZI HUO WA MH. RAIS


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, akiongelea utenguzi wa Mkurugenzi wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea uliofanywa na Rais Magufuli na pia kusimamishwa kazi kwa watumishi wanne wa TAKUKURU ambao waliomba kibali cha kusafiri nje ya nchi na kukataliwa lakini wakaamua kusafiri kibabe. (AUDIO) Usisahau kuSHARE na marafiki
Posted by East Africa Television (EATV) on Wednesday, December 16, 2015


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo