Picha 25 za maporomoko ya udongo yaliyofunga barabara wilayani Makete

Mvua zinazoendelea kunyesha Makete mkoani Njombe zimesababisha madhara ya barabara kujifunga eneo la Kisajanilo Iwawa Makete baada ya udongo kuporomoka na kuifunga barabara hiyo itokayo Makete mjini Kwenda Bulongwa

Juhudi za wilaya ya Makete kuwasiliana na Mkoa wa Njombe wakiongozwa na mkuu wa wilaya hiyo Mh Daud Yassin Zilizaa matunda na kusababisha TANROAD mkoa wa njombe kufika na katapila lililoondoa kifusi hicho na kuifanya barabara hiyo kupitika kama mwanzoni

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Desemba 9 mwaka huu, angalia picha za tukio hilo
Mkuu wa wilaya ya Makete Daud Yassin (wa kwanza kushoto) akiwa na mhandisi wa ujenzi wilaya ya Makete Bw TEmbo na viongozi wa TANROAD mkoa wa Njombe wakiwa eneo la tukio
Katapila likiwa kazini kuondoa kifusi





Magari yakianza kupita

Mkuu wa wilaya ya makete Daud Yassin akifuatilia kwa ukaribu zoezi hilo hadi lilipokamilika


Baadhi ya abiria waliokwama wakiwa eneo la tukio







Mkuu wa wilaya ya Makete Daud Yassin akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo

Viongozi hao wakiangalia sehemu nyingine inayoonekana kumomonyoka


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo