"Hakutakuwa na Fiesta Mwaka Huu, Tumsapoti Magufuli" yasema Clouds Media

Mkurugenzi wa Clouds Media Group ambao ni waandaaji wa tamasha la Fiesta, Ruge Mutahaba amesema kuwa tamasha hilo halitakuwepo mwaka huu.

Amesema wameamua kuahirisha kufanya tamasha hilo mwaka huu kutokana na ufinyu wa muda uliobaki hasa baada ya kupisha kipindi cha uchaguzi.

“Tulijua tukimaliza kampeni tutafanya kwa mikoa michache lakini tumeona kwamba hakuna kitu kizuri kama kumsupport mheshimiwa Magufuli , hebu sasa hivi turudi kwanza tutulie tuache hii amsha amsha aliyoanza nayo ianze kufanya kazi tujipange kwaajili ya Fiesta 15 ambayo itafanyika mwaka kesho,” Ruge aliiambia XXL ya Clouds Fm.

“Tutakuwa tunafikisha miaka 15 ya Fiesta na nina uhakika itakuwa na ukubwa inayostahili kuliko kufanya kitu kidogo mwaka huu. Tumeona tuache mwaka kesho mikoa 15, miaka 15 ya Fiesta itakuwa kubwa zaidi. Hapa Kazi imebidi iivae Fiesta pia,” alisema.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo