Akamatwa akiiba mtoto mchanga mkoani Njombe

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Flora Msigwa anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Njombe kwa tuhuma za kuiba mtoto wa Irene Kayombo mkazi wa Njombe
 
Kamanda wa polisi mkoani Njombe Wilbroad Mutafungwa amekiri kumshikilia mwanamke huyo na kwamba mara baada ya kupewa taarifa za mama huyo kuwa na mtoto mchanga wasamaria wema walitoa taarifa kituo cha polisi Makambako ambako jeshi hilo lilifika kwake na kumkuta mtoto huyo akiwa naye na alikiri kutenda kosa hilo.

Mtuhumiwa aliiba mtoto huyo katika hospitali ya Kibena Njombe ambapo mama wa mtoto alikuwa akimuuguza dada yake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo