Waziri aliyeangushwa ubunge azungumzia ya moyoni mwake

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi amesema pamoja na kuanguka kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, bado anayo nafasi ya kushiriki kuleta maendeleo ya Jimbo la Mbozi.
 
Zambi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya, alisema hatosita kutoa ushirikiano pale atakapohitajika na mbunge mpya wa jimbo hilo, Pascal Haonga aliyeshinda kupitia Chadema.
 
Zambi aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbozi kwa vipindi viwili na kuingia katika kinyang’anyiro kuwania muhula wa tatu, alisema anayo nafasi kubwa ndani ya jamii na hivyo anayo fursa ya kuendelea kushirikiana na wananchi.
 
“Sitosita kumpa ushirikiano mbunge wa Chadema. Lengo letu ni moja kuwaletea maendeleo wananchia,” alisema.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo