Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amemsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 27.Nov 2015 Kamishna mkuu wa TRA nchini ndugu Rished Bade kufuatia ziara ya kushitukiza ya waziri mkuu Mh. Majaliwa Kassimu Majaliwa mapema leo asubuhi baada ya kubaini bandari ya Dar es salaam kupitisha makontena zaidi ya miatatu na kusababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 80.
Rais Dkt John Pombe Magufuli amemteua Katibu mtendaji wa tume ya mipango Dkt. Philip Mpango kukaimu nafasi hiyo taarifa hiyo iliyosomwa na Katibu mkuu Kingozi Balozi Ombeni Sefue ikiwataka maofisa wote wa TRA kutosafiri nje ya nchi mpaka pale uchunguzi dhidi yao utakapo kamilika.