Hawa ndio vigogo wa TRA waliofutwa kazi na waziri mkuu Majaliwa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar es Salaam mapema leo na kubaini upotevu wa makontena 349.

 Waziri Mkuu amebaini upotevu wa makontena hayo ambayo yana thamani ya zaidi ya shilling bilioni 80, na kuagiza kufutwa kazi mara moja kwa maafisa waliohusika na upotevu huo.

Majaliwa amewasimamisha kazi Kamishna wa Kodi, Tiagi Masamaki pamona na Habibu Mpozya wa kitengo cha huduma kwa wateja.

Uamuzi huo wa Waziri Mkuu umekuja baada ya kubaini kuwa katika kumbukumbu za Mamlaka ya Bandari kuna taarifa ya makontena 349 yenye thamani ya shilingi bilioni 80 lakini taarifa hizo hazipo kwenye kumbukumbu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Waziri Mkuu ameelekeza Polisi kuwakamata maafisa wote waliohusika na sakata hilo kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo