Baba atiwa mbaroni wakati akimbaka mtoto wake huko Sumbawanga

Watoto wawili wenye umri wa miaka 13 wamebakwa kwa nyakati tofauti, huku mmoja akidaiwa kufanyiwa ukatili huo na baba yake wa kambo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema tukio hilo lilitokea eneo la Mtaa wa Kashai alfajiri ya Novemba 15 mwaka huu. 

Alidai kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa alitoka chumbani kwake alikokuwa amelala na mkewe na kwenda chumba alichokuwa amelala binti huyo ambaye alimwamsha na kumpeleka kwenye pagala lililokuwa jirani na nyumba yao ambako alimbaka. 

“Kutokana na maumivu, mtoto huyo alipiga kelele, mama yake na majirani walimsikia wakatoka na kumkuta mtuhumiwa akiendelea kufanya kitendo hicho,” alidai. Alisema polisi wanamshikilia mtuhumiwa kwa uchunguzi kabla ya kumfikisha mahakamani mara watakapoukamilisha.

 Katika tukio lingine, polisi wanamsaka mwendesha bajaji mmoja anayedaiwa kumbaka binti mwingine wa miaka 13. 

Kamanda Mwaruanda alisema binti huyo alifanyiwa kitendo hicho Novemba 18, saa 10 jioni baada ya kukodi bajaji hiyo kutokea Soko la Mandela ili impeleke mtaa wa Edeni B. 

Alidai kuwa wakiwa njiani, ghafla dereva huyo alibadili njia na kumpeleka kwenye kichaka kilicho karibu na Kanisa la Hija. “Huko alimbaka na kumtelekeza hapo kabla ya kutokomea kusikojulikana,” alidai Kamanda huyo. 

Alisema tayari watoto hao wameshapatiwa matibabu Hospitali ya Mkoa Sumbawanga na hali zao zinaendelea vizuri. “Bado tunaendelea kumsaka mtuhumiwa mara tutakapomtia mbaroni tutamfikisha mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake ili kukomesha vitendo hivi,” alisema. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo