Washindana kupiga "push up" kama Magufuli mbele ya Mgombea

Wanaume kadhaa wa eneo la Sirari, jana walishindana kupiga ‘pushapu’ mbele ya mgombea mwenza wa urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan baada ya kuvutiwa na sera zake. 

Hatua ya wanaume hao ilisababisha kuvuma kwa kelele za shangwe katika uwanja wa Tarafa, mahali mkutano wa kampeni wa mgombea huyo ulipofanyika. 

Kabla ya ‘pushapu’ hizo ambazo zimepachikwa jina la Magufulika, Samia alinadi Ilani ya CCM akisema imejipanga kuwawezesha wananchi kupiga hatua mbele kiuchumi. 

Alisema pamoja na kukusudia kujenga viwanda, pia wanakusudia kuboresha maeneo yenye fursa za kibiashara. 

“Tunajua Soko la Remangwe bado linajengwa, tutahakikisha tunalikamilisha ili kutanua fursa za kibiashara kwa Sirari na Mkoa wa Mara kwa ujumla,” alisema Samia. 

Pia, alisema wamepanga watakapofanikiwa kuingia madarakani kuanzisha mamlaka ya biashara ndogo itakayosimamia shughuli kama vile za mama lishe na waendesha bodaboda. “Tunataka wajiunge katika vikundi ili waweze kupata mikopo itakayotolewa kwa udhamini maalumu wa Serikali, hivyo itasaidia kukuza mitaji na biashara zao kwa ujumla,” alisema. 

Samia alisema wanakusudia kuwatengea wafanyabiashara hao maeneo maalumu ya kufanyia shughuli zao ili kuwaepusha na kero ya askari mgambo. 

Mgombea huyo mwenza alisema wamepanga kuwajengea waendesha bodaboda mazingira mazuri ya kazi, kwa kutenga vijiwe kwenye kila kituo na kuviwekea rangi maalumu kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyofanywa, hasa maeneo ya mjini. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo