Mgombea anusurika kwenye ajali ya gari Kigoma

Mgombea ubunge wa ACT-Wazalendo katika Jimbo la Manyovu mkoani Kigoma, Goodluck Kimali amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kupinduka likiwa kwenye msafara wa Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe. 

Ajali hiyo ilitokea katika Kijiji cha Nyalulanga, Kata ya Busunzu wilayani Kibondo katika Mkoa wa Kigoma, juzi, usiku. 

Tukio hilo lilihusisha gari aina ya Nissan katika msafara uliokuwa na magari manane ukitoka Kasulu kwenda Kibondo, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya kampeni ya chama hicho katika majimbo manane mkoani hapa. 

Zitto alisema ajali hiyo ilitokea saa mbili usiku na kabla ya kupinduka, gari hilo lilipata pancha tairi moja la mbele likiwa

Msafara huo ulihusisha wagombea wote wanane wa majimbo ya Mkoa wa Kigoma ambao unapita kila jimbo kufanya mikutano kwenye kata na jioni hukutana kufanya mkutano katika eneo moja. Dereva wa gari hilo alisema chanzo cha ajali ni pancha iliyotokea kwenye tairi la mbele, upande wa kulia, na kusababisha ‘kumvutia’ porini na kupinduka. 

Baada ya ajali hiyo iliyosababisha michubuko kwa watu wanne, majeruhi hao walichukuliwa na kupelekwa mjini Kibondo kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza na taarifa zilizopatikana baadaye zilieleza kuwa waliendelea na ziara katika Jimbo la Muhambwe wilayani Kibondo.  


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo