Walimu Mbinga waongezewa majukumu na mkuu wa wilaya kuhusu wanafunzi wao

Wilaya ya mbinga mkoani Ruvuma  imeweka  utaratibu wa watendaji wa kata na vijiji kufuatilia mahudhhurio ya wanafunzi shuleni  ili  kudhibiti utoro kwa wanafunzi na kumpunguzia  mzigo   mwalimu  kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu  wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ya mbinga Bi.Senyi  Ngaga amebainisha hayo  wakati akizungumza kwenye mkutano wa  wakuu wa shule za sekondari kanda  ya nyanda za juu kusini uliofanyika mjini mbinga ambapo katika mpango  huo watendaji wa kata wanafuatilia mahudhurio ya wanafunzi wa sekondari  na watendaji wa vijiji wanafuatilia mahudhurio ya wanafunzi wa shule za msingi.
 
Kwa upande wao walimu wameiomba serikali kulipa malimbikizo na madai ya walimu na kuborsha mazingira ya shule.
 
Naye mwenyekiti wa wakuu wa shule za msingi kanda ya nyanda za juu kusini Bw.Ponsiano Ngunguru  kupunguza changamoto katika shule za sekondari.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo