Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mama Sihaba Nkinga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tanzania Media Foundation - Mfuko wa Habari Tanzania - TMF) uliyofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam. Mfuko huu unachukua nafasi ya Tanzania Media Fund 
Mkurugenzi wa Shirika la habari la Daraja Bw. Simon Mkina akipokea tuzo wakati wa uzinduzi huo wa Mfuko wa Habari Tanzania
Mkurugenzi wa TMF Bw. Ernest Sungura akizungumza na wadau mbalimbali waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) uliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam
Mrisho Mpoto akitumbuiza wakati wa uzinduzi wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) iliyofanyika leo katika ukumbi wa Millenium Tower jijjini Dar Es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya TMF Mama Halima Shariff akitoa neno la shukurani baada ya bodi hiyo kuzinduliwa usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam. .
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mama Sihaba Nkinga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wapya wa Bodi ya TMF na watendaji wa mfuko huo usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Edwin Moshi