Nyosso apewa kifungo na faini juu baada ya kumdhalilisha Bocco

Kikao cha Kamati ya nidhamu ya TFF kilichokutana ndani ya saa 72, kimefungia nahodha wa Mbeya City, Juma Said Nyosso kucheza soka kwa miaka miwili.


Pamoja na miaka hiyo miwili, Nyosso ametozwa faini ya Sh milioni mbili kutokana na kitendo chake cha kumshika makalio nahodha wa Azam FC, John Bocco.


Hii ni mara ya pili kwa Nyosso kushiriki katika tukio, mara ya kwanza alimtomasa Elius Maguli wakati akiichezea Simba.

Kutokana na picha ilivyochapishwa kwenye gazeti la Championi na SALEHJEMBE akafungiwa kucheza mechi nane.


Baada ya hapo, Nyosso aliwaomba radhi Watanzania pamoja na wapenda soka wote, lakini bado amerudia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo