Uongozi wa ITV na Redio One unakanusha taarifa za uzushi zilizoenezwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii zikimhusisha mwandishi wetu kuwa ameshiriki kuanzisha matawi bandia ya Chadema katika maeneo ya Tandale na kuwapanga vijana wa chama cha Mapinduzi kwa kuwavalisha nguo za Chadema kwa lengo la kususha bendera za Chadema na kupandisha ya CCM.
Taarifa hizo ni uzushi na zenye nia ovu ya kumdhalilisha mwandishi huyo .
ITV ni kituo makini chenye kuzingatia weledi ambacho hakiwezi kutumiwa au kukubali kutumika kufanikisha propaganda hizo.
Tunawasihi watazamaji na wasikilizaji wetu kuzipuuza na kuendelea kuwa na imani na watendaji wa kituo hiki.
