Ya nini malumbano? ACT - Wazalendo waamua kuzindulia kamepni zao kitaifa Mbagala

Chama cha ACT – Wazalendo kitazindua kampeni zake za uchaguzi kwa kuwatambulisha wagombea wote wa ubunge waliosimamishwa kwenye majimbo ya Tanzania –Bara na Zanzibar. Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Agosti 30 katika Uwanja vya Zakhem Mbagala, wilayani Temeke kuanzia saa nne asubuhi.
Katibu wa Mipango na Mikakati wa ACT – Wazalendo, Habibu Mchange aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba maandalizi ya uzinduzi huo yanaendelea vyema na kwamba hafla hiyo itahudhuriwa na viongozi wote wa kitaifa wa chama hicho wakiwamo Kiongozi wa Chama, Zitto Kabwe na Mwenyekiti wake, Anna Mghwira ambaye pia ni mgombea urais.
“Baada ya mwenyekiti wetu, Mama Mghwira kuchukua fomu ya kugombea urais, Watanzania wamekuwa na shauku ya kutaka kujua mustakabali wetu kuelekea Uchaguzi Mkuu,” alisema na kuongeza: “Hivyo basi tunawakaribisha wananchi wote siku hiyo waje kushuhudia kampeni za kisayansi. Ndiyo maana tumeamua kuwaita wagombea ubunge wote kuhudhuria na kuwatambulisha rasmi kwa Watanzania.”
Alisema ACT – Wazalendo imejipanga kuchukua dola na kuleta siasa safi, tofauti na vyama vingine akisisitiza kuwa kina nia ya dhati ya kuwaletea maendeleo ya Watanzania. Hivyo kuwataka wananchi kuhudhuria.
Alisema katika siku ya uzinduzi, kwa mara ya kwanza wabunge waliohama kutoka vyama vya CCM, CUF na Chadema watazungumza, pia wataendelea kuinadi ilani ya uchaguzi wa chama hicho. Alisisitiza kuinadi kaulimbiu ya chama hicho ya utu, uadilifu na uzalendo.
Katibu wa Fedha na Rasilimali ya chama hicho, Peter Mwambuja alisema pia kimejipanga kufanya siasa za malengo na masuala kwa maendeleo ya Watanzania siyo kupiga propaganda.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo