Wakulima katika bonde la UYOLE waanza kunufaika na kilimo cha umwagiliaji

Baadhi ya Wakulima katika  Bonde la UYOLE lililopo nje kidogo ya Mji wa MBEYA wameanza kunufaika na Mradi wa Umwagiliaji maji wa IGANJO.

Miundombinu ya mradi huo imejengwa na serikali kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Milioni 190.

Mwenyekiti wa Ushirika wa Umwagiliaji Maji Bonde la UYOLE  - JOHN SODA amesema kuwa ujenzi wa mradi huo umekamilika kwa asilimia 80 na  asilimia 20 zilizobaki zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Utekelezaji wa mradi huo  wa Umwagiliaji maji wa IGANJO umelenga zaidi kilimo cha zao la Viazi Mviringo na Mbogamboga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo