Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe ameshauriwa na madaktari apumzike baada ya jana kukimbizwa hospitali ya Taifa Muhimbili, wakati alipojisikia vibaya ghafla akiwa kwenye msafara wa kumsindikiza mgombea urais wao kuchukua fomu za kugombea urais ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Akiongea na waandishi wa habari juu ya afya ya Mhe. Mbowe, Daktari Bingwa Magonjwa ya Moyo, Shem Tulizo Sanga amesema Mhe. Mbowe anaonekana kuchoka sana kufuatia shughuli ambazo amekuwa akizifanya mfululizo hivyo anahitaji kupumzika ili kurejea katika hali yake ya afya ya kawaida.