"Nikichukua nchi wanaoiba dawa hospitalini watakoma" asema Dkt Magufuli

Akihutubia katika mkutano wa hadhara wilayani Nkasi Mkoani Rukwa Magufuli amesema endapo atachaguliwa wahudumu wanaoiba dawa katika hospitali nchini atawashughulikia kwa mujibu wa sheria ili kukomesha hali hiyo.

Dkt. Magufuli ameongeza kuwa tabia ya watu kwenda hospitali kutibiwa na kuambiwa wakanunue dawa kwenye maduka binafsi kwa kuwa vituo vya afya havina dawa hizo ataikomesha mara moja.

Aidha Waziri Magufuli amesema anafahamu bayana shida za wananchi wa mikoa hiyo zikiwemo za barabara za lami, umeme, maji, elimu, uhuru wa kufanya biashara na migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji na kwamba atatatua matatizo hayo iwapo wananchi watampa ridhaa ya kuingia ikulu mwezi Oktoba.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo