Mtangazaji alivyovamiwa na kuuawa ndani ya Studio

Hili ni tukio ambalo limechukua sana headlines mitandaoni na kwenye Vyombo vya Habari vikubwa vya Kimataifa Duniani, mtangazaji kavamiwa akiwa anarekodi show yake kwenye Kituo cha Radio Brazil !!
Kinachoibua maswali kwa upande mwingine ni kuhusu nani kahusika na mauaji hayo? wauaji waliingia mpaka ndani na kuua alafu wakafanikiwa kutoka salama, mtangazaji Gleydson Carvalho kauawa kwa kupigwa Risasi tatu kichwani na kifuani.
Wauaji hao walivamia na kumzidi nguvu mtu wa mapokezi, wakamkamata producer wa show akalazimishwa kuingia chini ya meza… alafu wakamalizia kwa kumuua mtangazaji huyo ambaye alikuwa maarufu sana kutokana na kuikosoa Serikali kushindwa kupambana na tatizo la Rushwa.

Angalia video hii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo