Mwenyekiti mwenza wa umoja wa baadhi ya vyama vya siasa vya upinzani JAMES MBATIA amewashauri wagombea wa nafasi mbalimbali za kisasa kunadi sera kwa wananchi badala ya kunyooshena vidole.
Mbatia ameyasema hayo jijini DSM katika Mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema watanzania ni wamoja na wanahitaji kusikia sera kutoka kwa wagombea na siyo vinginevyo.
Kampeni za uchaguzi zitarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe ishirini na mbili baada ya kukamilika kwa nafasi za uteuzi.