Kauli 19 za Mbowe alizosema leo kumhusu Edward Lowassa

Mbowe: Tunaamini tulianza na Mungu kwenye safari yetu, tunaimani tunaendelea na mungu na tutamaliza na mungu

Mbowe: Tunaamini kila linalotokea ni mpango wa Mungu.

Mbowe: Tumepigana kwa miaka 25 kufika hapa tulipo leo, haikuwa kitu rahisi, wapo waliopata matatizo mengi.

Mbowe: Lakini wako tuliowaita magamba, nao wakaamua kimagamba magamba wakafunga safari yao ya matumaini kutafuta haki

Mbowe: Tuna kila sababu ya kuwaunga mkono, tuna kila sababu ya kuwakaribisha kwetu ili ndoto hiyo itimie.

Mbowe: Sisemi wanaokuja CHADEMA leo wote wana dhambi, hata sisi tulioko CHADEMA leo tuna mapungufu yetu.

Mbowe: Kwahiyo nichukue fursa hii kumkaribisha Edward Lowassa, hawa ndio wenye chama chao sisi wengine wabeba dhamana tu

Mbowe: Kwenye CHADEMA hakuna aliye mkubwa kuliko chama chetu, tukikubaliana tunasonga tunasonga tu.

Mbowe:Yale mabaya mliyokuwa nayo kwenye chama chenu cha zamani tumeyasamehe, tunaomba mtuletee yale mazuri mliokuwa

Mbowe: Hadi siku ya jana Mgombea Mwenza wa CHADEMA alikuwa Waziri Zanzibar lakini ameona ajiuzulu kujiunga na sisi.

Mbowe: Kwa sababu tuna uhakika wa kukamata madaraka ya nchi hii, hiyo sheria tutaibadilisha 'faster'

Mbowe: Naomba nimhakikishie Mh. Duni, yuko kwenye mikono salama na atafanya kazi kikamanda

Mbowe: Ngoja nisome historia ya Edward Lowassa kwa kujidai kidogo, nifute jasho na ninywe maji.

Mbowe: Mh. Lowassa amemuoa mama Regina Lowassa na kujaliwa kupata watoto watano.

Mbowe: Mh. Lowassa ni shabiki mkubwa wa michezo na alikuwa mchezaji mkubwa wa mpira wa kikapu. 'basketball'
Mbowe: Kamati kuu ilifanya utafiti tena ilifanya utafiti kwa vikao vingi mfululizo

Mbowe: Tafiti zetu zilituambia kwamba Mh. Lowassa akipeperusha bendera yetu ndani ya UKAWA, ndoto ya Taifa hili inatimia.

Mbowe: Wote tuliafikiana na kukubaliana kwamba tumpitishe Lowassa, akiwemo katibu Mkuu Dk. Slaa.

Mbowe: Mapendekezo ya Baraza Kuu yamekubali LOWASSA na Haji Duni wapeperushe Bendera ya UKAWA kwenye Urais

Mbowe: Tumependekeza Maalim Seif pekee wa chama cha CUF awe mgombea wa Urais Zanzibar akiwakilisha UKAWA.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo