Breaking News: Wingu Jeusi CUF, mkutano wake na wanahabari waahirishwa ghafla

Chama cha wananchi CUF kimeahirisha mkutano wake na waandishi wa habari ulioitishwa na mwenyekiti wa chama hicho taifa Prof. Ibrahimu Lipumba

Taarifa za kuahirishwa mkutano huo zimetolewa na naibu katibu Mkuu Magdalena Sakaya amewaomba radhi waandishi wa habari waliofika kwenye makao makuu ya Chama hicho Buguruni jijini DSM ambapo zimeonekana kuzua hali ya sintofahamu

Amesema mkutano huo umeahirishwa na hawafahamu ni nini alichokuwa akizungumze Prof Lipumba lakini kwa hivi sasa Lipumba anazungumza na wazee wa chama hicho kwa kuwa wanataka kufahamu ni kitu gani angekwenda kukizungumza kabla hajakwenda kukizungumza

Katika tukio jingine mwandishi wa habari na mpiga picha wa magazeti ya UHURU Immanuel Ndege amejeruhiwa kwa kukatwa na feni kichwani katika ofsis hizo za CUF wakati akipiga picha kinachoendelea katika mkutano huo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo