Leo kulikuwa na upigaji kura ya maoni kuwapata wagombea wa Ubunge na udiwani katika majimbo na kata mbalimbali nchi nzima kupitia chama cha mapinduzi CCM
Yafuatayo ni matokeo ya uchaguzi huo kwa kata ya Tandala wilaya ya Makete mkoa wa Njombe kwa ngazi ya udiwani na Ubunge kama yalivyotolewa na msimamizi wa uchaguzi kata ya tandala Bw. Yusuph Kisimbilo Sanga
1. Udiwani
Walikuwepo wagombea wawili ambapo mtetezi wa nafasi hiyo Bw. Egnatio Mtawa amepata kura 675 dhidi ya mshindani wake Bw. Yusuph Ilomo aliyepata kura 79
2. Ubunge (kata ya Tandala tu)
Prof Norman Sigalla amepata kura 481, Dr. Binilith Mahenge anayetetea nafasi yake amepata kura 200, Boniki Mhami 36, Fabian Nking'wa 32, na Lufunyo Nkinda 11
Matokeo halisi ya ubunge bado yanakusanywa na yakikamilika utayapata hapa hapa
