Nimekutana na stori kutoka Iceland inayomhusu mwanaume mmoja kutoka Nigeriaambaye amekamatwa na polisi kwa madai ya kusambaza ugonjwa wa UKIMWI kwa makusudi.
Mwanaume huyo ambaye jina lake bado halijajulikana ni raia kutoka Nigeria ambaye amekuwa akijaribu kupata uraia wa sehemu hiyo toka mwaka 2014.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kituo cha police cha Iceland, Iceland Review Reportimesema:
>>>“sehemu kubwa ya upelelezi tunaoufanya sasa hivi ni kujua kama wanawake wengine wamekutana kimwili na huyu mwanaume zaidi ya ile idadi tulionayo kwenye ripoti zetu…”<<< Iceland Police.
>>>“taarifa zingine za matukio ya kiualifu ya mwanaume huyu bado zinakusanywa. Kwa sasa shitaka kubwa dhidi yake ni kujihusisha na vitendo vya kimapenzi kwa nia ya kusambabza ugonjwa wa UKIMWI- kitendo ambacho kikithibitishwa kitakuwa ni kinyume na sheria zetu za nchi”. <<< Iceland Police.
