ACT - Wazalendo kuishitaki CHADEMA

Chama cha ACT – Wazalendo kimewaonya chama cha Demokrasia na Maendeleo kuacha kuwafanyia vurugu katika mikusanyiko yao pamoja na kushuka bedera za chama hicho.
Hayo yameelezwa na Katibu Mipango na Mikakati Habibu Mchange ambapo amedai kuwa chama cha Chadema kimevunja matawi baadhi ya maeneo nchini hivyo na kuwatia hasara kubwa.
Mchange amesema kama tabia hiyo ikiendelea basi ni wazi watawachukulia hatua za kisheria wapinzani wao hao.
Pia chama cha ACT kimetangaza rasmi kwamba kitaanza kampeni zake za kusaka urais,ubunge na madiwani siku ya agosti 30 katika viwanja vya Mbagala Zakhem – Jijini Dar es Salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo