Wazirai na kukimbizwa hospitali kwa kukosa pombe ya kunywa..!!

Watu wanne wamezirai na kukimbizwa katika hospitali ya Nyahururu, Kenya baada ya kuzidiwa kwa kukosa pombe.
Kulingana na madaktari katika hospitali hiyo, wanaume hao walilazwa baada ya juhudi za kuwarejeshea fahamu kwa kuwanywesha maziwa kugonga mwamba.
Ofisa matibabu katika hospitali hiyo ambaye alikataa jina lake kutajwa alisema  wanaume hao walianguka na kukosa fahamu baada ya kukosa pombe walioachishwa gafla.
“Kawaida mtu akiwa na mazoea ya kunywa pombe kisha kumwachisha ghafla mwili huhisi kukosekana kwa kiungo muhimu”.
Alisema kwa sasa watu hao wanaendelea vizuri na matibabu  na kufuatia tukio hilo walevi waliokuwa kwenye kampeni ya kuacha ulevi wameishutuma Serikali kwa hatua ya kuwalazimisha kuacha pombe gafla.
Wakazi wengi wa eneo hilo walisema  hawawezi kufanya kazi bila kunywa pombe kwa kuwa inawasaidia kuwaongezea ari ya kujituma


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo