Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ANGELA KAIRUKI amawaagiza Watendaji wa wizara hiyo kuangalia namna ya kuboresha makazi ya Watumishi wa Chuo cha Ardhi TABORA, ambayo kwa sasa yana hali duni.
KAIRUKI ametoa agizo hilo baada ya kutembelea nyumba za Watumishi hao ambazo zimejengwa kwa mabati na kusema kuwa nyumba hizo hazifai kwa makazi.