Halmashauri ya wilaya ya MBOZI imesitisha malipo kwa wakandarasi wake wawili kampuni ya KERRY COMPANY na MSUKWA GENERAL COMPANY zilizopewa tenda za ujenzi wa barabara kiwango cha changarawe ndani ya halmashauri hiyo
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo Mwenyekiti wa halmashauri ya MBOZI, ERICK AMBASISYE amesema hakuridhishwa na ujenzi wa barabara hizo ambazo ni ile ya Inanda mpaka Chindi pamoja na barabara ya kutoka Vwawa kwenda Igamba ambazo amebainishwa zote kujengwa chini ya kiwango