WAHAMIAJI HARAMU WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA KAGERA KUKIONA CHA MTEMA KUNI

Mkuu wa mkoa wa Kagera John Mongela ametoa onyo la mwisho kwa wahamiaji haramu wote walijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kuwa watawajibisha kisheria ikiwa nipamoja na kutumikia kifungo cha miezi sita jera bila huruma.

Mkuu wa mkoa wa Kagera John Mongela amesema hayo mara baada ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura katika kituo cha uwanja wa ndege mjini Bukoba ambapo amewataka wahamiaji haramu waliojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kinyume na sheria kujisalimisha mara moja kabla sheria haija chukua mkondo wake.
 
Hata hivyo mkuu wa mkoa wa Kagera John Mongela amesema Tanzania sio shamba la bibi  kuwa kila mtu anaweza kufanya anachotaka kinyume na taratibu za nchi nakwamba serikali haiwezi kuwavumilia raia wanaoingia nchini kunyume na sheria nakujificha kwa kivuli cha vyama vya siasa huku akiwataka wananchi kutosita katika kuwafichua wahamiaji haramu wanaoshirika katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. 
 
Hali hiyo imejitokeza kufuatia baadhi ya vituo vya kuandikisha watu katika daftari la kudumu la wapiga kura kubainika kuwa na wimbi la wahamiaji haramu na hasa katika wilaya ya Kyrwa ambayo ikopembezoni mwa nchi ambayo pia imepakana na nchi jirani za Rwanda na Uganda.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo