DKT SLAA AITUPIA KAULI NZITO TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI, ASEMA ANAONGEA KWA MARA YA MWISHO KIFUATACHO NI.......!!!!

Katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo, Chadema, Dk. Wilbrod Slaa amemtaka mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi, NEC, jaji mstaafu Damian Lubuva kutoa kauli na msimamo wa tume hiyo juu ya hatma ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kuhusu mahali watakapopigia kura ili haki za vijana hao isipotee.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mji wa vawa wilayani Mbozi, katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo, Chadema, Dk. Wilbrod Slaa amesema kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wako hatarini kupoteza haki yao ya kidemokrasia ya kupiga kura, kwa kuwa baadhi yao wamejiandikisha kwenye vituo wakati wakiwa vyuoni, lakini wakati wa kupiga kura vyuo hivyo vtakuwa vimefungwa na wanafunzi watakuwa majumbani mwao.
 
Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Mbeya, Joseph Mwachembe maarufu kwa jina la china amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya kuandikishia wapiga kura ili wakajiandikishe, huku pia akiiomba tume ya taifa ya uchaguzi kuongeza mashine za uandikishaji kwenye vituo ambavyo vina msongamano mkubwa wa wananchi wanaokwenda kujiandikisha.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa Chadema kanda ya nyanda za juu kusini, mchngaji Dk. Steven Simon Kimondo amesema kuwa monyoko mkubwa wa maadili ndio ambao umeliingiza taifa kwenye matatizo makubwa ikiwemo ubadhirifu wa mali za umma.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo