NEWS ALERT: SERIKALI YAMALIZA MGOGORO NA WAFANYABIASHARA JUU YA MATUMIZI YA EFDs


Waziri wa Fedha Mh. Saada Mkuya Salum akiwa katika picha ya pamoja 
wafanyabiashara alipotoa Taarifa ya muafaka uliofikiwa kati ya 
wafanyabiashara na serikali juu ya Matumizi ya Mashine za kielektroniki 
(EFDs) leo Jijini Dar es Salaam, Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya 
wafanyabishara Bw. Johnson Minja na Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi 
ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mzee Benard Mchovu
(Picha na Regnihaldah Mpete-TRA)


Na Anitha Jonas – MAELEZO.


Serikali yafikia muafaka katika mgogoro wake na wafanyabiashara juu ya 
matumizi ya mashine za kieletroniniki EFD’s.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Fedha Mhe.Saada Mkuya alipokuwa akitoa 
taarifa hiyo kwa vyombo vya habari juu ya Serikali kufikia muafaka wa 
makubaliano yaliyofanyika kwa ushirikiano wa Kamati kuu ya Taifa iliyoshirikisha  
wajumbe kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Viongozi wa Jumuiya 
ya wafanyabiashara katika ngazi ya Taifa.


“Matumizi ya mashine za EFD yalipoanza yalileta changamoto kwa 
wafanyabiashara ,hivyo niliunda kamati ya kitaifa pamoja na kamati katika ngazi 
za Mikoa na Wilaya pamoja na wenyeviti wakuu wa mikoa kutafuta suluhu la 
suala hili”alisema Mhe. Mkuya.


Waziri Mkuya aliendelea kusema Kamati imetoa mapendekezo mbalimbali kwa 
Serikali ikiwemo ya muda mfupi ambayo wameshaanza kuyafanyia kazi na 
mengine ni yakisera ambayo yatahitaji muda mrefu yatafuata utaratibu 
unaopaswa katika utekelezaji wake,kwa ufuatiliaji na ushirikiano wa karibu,kupitia 
kamati ya Kitaifa itakayodumu kwa kipindi cha miaka miwili.



Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini Bw.Johnson Minja 
aliipongeza serikali kwa kubali kukaa meza moja na wafanyabiashara katika 
kutatua mgogoro huo uliyokuwepo katika matumizi ya mashine za EFD na 
kuakukubali kupokea changamoto za wafanyabiashara na kuahidi kuzifanyia kazi.

“Serikali imekubali kupitia mfumo wa utozwaji kodi kuanzia ngazi ya bandarini na 
kuongeza uwazi ilikuleta uelewa kwa wafanyabiashara na kuepuka kutozwa kodi 
kubwa kutoka na kukosa uelewa wa gharama za ulipaji kodi”,alisema Bw.Minja.



Aidha Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ya wafanyabiashara aliendelea kusema ni 
wajibu wa kila mmoja kulipa kodi na hii ni kwa maendeleo ya nchi na pia ni kosa 
kwa mfanyabiashara yoyote kuendesha biashara yake bila kuwa na namba ya 
utambulisho wa mlipakodi (Tin Number), tunataka namba ya walipakodi iendelee 
kuongezeka na kuondoa kabisa wafanyabiashara wasio lipa kodi.


Mbali na hayo nae Kamishana Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Rished Bade 
aliipongeza kamati kwa kuweza kufika mwafaka na kuweza kuzitambua 
changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiwasumbua wafanyabiashara na ameahidi 
,kuwa ofisi yake itaendelea kuwawajibisha watu wote wanao kiuka taratibu za 
ulipaji kodi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo