AFISA MKUBWA HUKO ZANZIBAR KUSHTAKIWA KWA KOSA LA KUZUIA WANANCHI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Ikiwa imebaki miezi michache kufanyika uchaguzi mkuu nchni hali ya kisiasa viziwani Zanzibar imeanza kuwa ya wasisi baada ya wabunge na wawakilishi wa chama cha wananchi-CUF-kujipanga kumburuza mahakamani jumatatu afisa mdhamini wa vitambulisho vya mzanzibar mkazi Pemba na wa wilaya ya mkoani kwa kuzuia haki ya kikatiba wananchi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.

Wakizungumza na waandishi wa habari bungeni mjini Dodoma wabunge wa chama cha wananchi-CUF- wamesema watu zaidi ya 400 wamenyimwa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura katika wilaya ya mkoani, jimbo la Kiwani na, jimbo la Mkanyageni pamoja na wengine kutoka Unguja kutokana vikwazo mbalimbali ikiweo kutopewa vitambulisho vya mzanzibar mkazi. 
 
Baadhi ya wabunge wamewatuhumu baadhi ya wakuu wa wilaya na mikoa visiwani Zanzibar kwa kukabidhiwa jukumu la kuhakikisha baadhi ya wanachama na wafuasi wa CUF haingizwi majina yao katika daftari ya wapiga kura lengo likiwa ni kupunguza kura zao katika uchaguzi mkuu baada ya kugundua chama cha wananchi CUF kinawananchi wengi.
 
Wakati hayo yakijitokeza huko Zanzibar, kwa upande wa Tanzania bara baadhi ya wabunge wa majimbo yaliyo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro wamemtaka rais Jakaya Kikwete kumuwajibisha mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kwa tuhuma za kutumia madaraka yake vibaya, pamoja na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kumchunguza na watendaji wake dhidi ya tuhuma za kutumia fedha za umma katika kuanzisha kampuni binafsi. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo