KUNDI LA NYUKI LASABABISHA MAUAJI HUKO GEITA

Familia ya Diwani wa viti Maalum Mkoa wa Geita, Helena Mahona imevamiwa na kushambuliwa na nyuki ambao wamejeruhi mama mmoja na watoto wawili na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye ni shangazi wa Diwani huyo.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Joseph Majebele amesema alikuwa mbali na eneo hilo lakini akapewa taarifa ya kutokea kwa tukio hilo kwa njia ya simu na watu walioshuhudia.
Kamanda wa Polisi Geita, Peter Kakamba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu alifariki hapo hapo kwenye tukio huku majeruhi wakikimbizwa Hospitai na hali zao zinaendelea vizuri.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo