Akizunguza wakati wa zoezi la uteketezaji wa maji hayo ambao umefanyika katika eneo la Nyabange nje kidogo ya manispaa ya musoma, meneja msaidizi usimamiaji madeni na kodi za ndani wa TRA Bw Ernest Nkangaza,amesema kuwa maji hayo ya aina mbalimbali kutoka nchi hiyo jirani,yameingizwa nchini kwa njia za panya kati ya machi 9 na april 9 mwaka huu,na kusambazwa katika miji ya tarime na Musoma.
Naye afisa afya mkoa wa mara Bw.Bumija Mhando,amesema maji hayo kiafya si mazuri kwani yamegunduliwa kuwa ni maji ya kisima,ambayo ukaguzi wake haufahamiki na hivyo usalama wake unatia mashaka makubwa huku yakiwa na bei ndogo ukilinganisha na makampuni mengini.
Zoezi hilo la uteketezaji limefanywa na mamlaka ya mapato tanzania TRA Mkoa na idara ya afya likisimamiwa na maafisa kutoka jeshi la polisi na usalama wa taifa.