Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Bw. Justus Kamugisha amesema jeshi la polisi mkoa wa shinyanga limeanzisha operesheni kabambe ya kubaini na kuwakamata wahamiaji haramu wote na amewataka watanzania kuacha tabia ya kujihusisha na vitendo vya kuwahifadhi na kuwasafirisha watu hao na atakayekamatwa atafikishwa mahakamani na sheria itachukua mkondo wake.
watanzania wanaotuhumiwa kuwasafirisha wahamiaji hao haramu wamesema wao wametumwa kuwachukua watu hao mkoani mwanza na kuwafikisha katika mji wa kahama ambapo mtu mwingine atawachukua na kuwapeleka AFRICA KUSINI kupitia DAR-ES-SALAAM huku wahamiaji hao haramu wakidai kuwa wanasafiri kwenda AFRICA KUSINI kutafuta maisha mazuri kwakua nchini kwao hali ya maisha ni duni.