Hii ilimuacha kwenye wakati mgumu mwanamke mmoja Nairobi, baada ya kumfumania mama akiwa na mtoto wake..

Visa vya fumanizi vimeripotiwa tena.. hii imetoka Kenya, mwanamke amelalamika kwamba alimfumania mume wake na mwanamke ambaye alikuwa akimfahamu kuwa ni mama wa kambo wa mume wake.
Mama huyo ambae hana mahali pa kuishi amesema mume wake alimtelekeza pamoja na mtoto wake mdogo Nairobi.
Nikaona hapana.. hii maisha ya kuteseka sitaweza kuteseka na mzee wangu yupo ikabidi nikaja hapa Nakuru.. nikamfuata nikamkuta akiwa kwa mama yake.. wanaishi pamoja na mama yake” ; — alisema mwanamke huyo aliyemfumania mume wake.
Mwanamke huyo amesema alishangaa kuona anakaribishwa na mwanamke ambae alimfahamu kama mama wa kambo wa mume wake.
Vile alikuja akaingia tena mama akatandika vizuri kitanda wakalala kijana na mama yake.. wakalala kwa kitanda mimi nikatandikiwa chini nikalala.. asubuhi aliamka kutoka hapo vile aliamka akaenda, mimi hakunisemesha”; aliendelea kulalamika mwanamke huyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo