Diamond Akiri Kulifahamu Tatizo la Wema la Kutopata Mtoto Muda Mrefu, Adai Walijaribu Kulitafutia Tiba Lakini Hawakufanikiwa


Kwa muda mrefu, Diamond Platnumz alikuwa akilijua tatizo la mpenzi wake wa zamani Wema Sepetu la kutoshika mimba.

Akiongea na kipindi cha Ng’ari Ng’ari cha Clouds TV, Diamond alisema wakati wako pamoja waliwahi kuzunguka kwa wataalam mbalimbali kujaribu kupata tiba lakini hawakufanikiwa. Alisema ilifika wakati alimweleza tu kuwa akubali hali hiyo.

Kuhusu kile Wema alichokiandika kwenye Instagram hivi karibuni ambapo alieleza ukweli wa hali yake ya kutopata mtoto, Diamond alisema ujumbe huo ulimuumiza kama wengine walivyoumia.

Alisema alikuwa anafahamu jinsi watu wanavyomshambulia Wema kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kutopata mtoto na amemsifia kwa kuusema ukweli.

Hata hivyo aliwashauri watumiaji wa mtandao ya kijamii kuitumia vyema na sio kuitumia kuwatusi mastaa wao kwakuwa ni kweli maneno yao huwaumiza kama binadamu wengine.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo