ASKARI AUGUA KICHAA...KILICHOFUATIA KIKO HAPA

SoldierHii nimekuta kwenye mtandao wa gazeti maarufu Uingereza, linaitwa The Independent.. wameandika ripoti inayoonesha kwamba kuna kundi kubwa sana la Wanajeshi wa Uingereza ambao wamegundulika kuumwa ugonjwa wa akili, sababu ya ugonjwa huo ni dawa ambazo huwa zinatumiwa na Wanajeshi hao ili kuzuia wasipate maambukizi ya Malaria !!
Dawa hizo zinaitwa Mefloquine au jina jingine Lariam.. tayari toka 2008 mpaka leo kuna wanajeshi karibu 1,000 ambao walipata matatizo ya akili kutokana na kutumia dawa hizo wakiwa nje ya Uingereza kupigana vita.
Athari nyingine baada ya kutumia dawa hizo ni pamoja na kupata stress, na wengine wanajiua kabisa!
Alastair Duncan ni Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi hilo ambae aliwahi kwenda kwenye vita Sierra Leone, yeye ni mmoja ya walioathirika kwa kupata tatizo la akili baada ya kutumia dawa hizo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo