Alikataliwa kumuoa binti ambaye ni binamu yake, kilichotokea ni Hatari

Huwa inatokea Mwanaume anataka kumuoa mrembo flani lakini wazazi wa Mke mtarajiwa wanakataa mtoto wao kuolewa na jamaa labda kwa sababu za kidini, kitabia au kitabaka.
Basi hii imetokea Pakistani ambako Gul Ahmed Said amemuua Baba Mkwe mtarajiwa pamoja na watu wengine tisa wa familia yake baada ya kukataliwa kumuoa Binti wa Mzee huyo huko Charsadda.
Pakistan
Charsadda
Binti aliekua anataka kumuoa ni binamu yake ambapo Polisi wa Pakistani wamesema ugomvi ulianzia kwenye mabishano ya idadi ya dhahabu kwenye harusi.
Waliouwawa kwa risasi ni Watoto nane wa mzee huyo, mzee mwenyewe pamoja na mke wake ambapo Polisi bado wanaendelea kumtafuta Said ambaye amekua akitafutwa kutokana na mauaji mengine aliyoyafanya November 2014 kwa kuwaua Wazazi wake, kaka yake pamoja na shemeji yake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo