Watu wawili wanahofiwa kufariki dunia baada ya basi la Happy Nation lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Mbeya kupata ajali na kutumbukia kwenye mfereji katika eneo la Mikumi mkoani Morogoro.
Ajali hiyo imetokea jana mchana ikiwa ni muda mfupi baada ya ajali nyingine kutokea jana hiyo hiyo ikihusisha magari matatu kwenye Kijiji cha Mbweni, Handeni mkoani Tanga na kuua watu 10.